Showing posts with label dansi. Show all posts
Showing posts with label dansi. Show all posts

Tuesday, November 8, 2022

THE GREAT AHMAD KIPANDE OF KILWA JAZZ BAND

 THIS BLOG WILL NOW ALSO BE PUBLISHING ARTICLES IN ENGLISH. TODAY WE BEGIN WITH THIS ARTICLE ON THE GREAT SAXOPHONE PLAYER AND BAND LEADER THE LATE AHMAD KIPANDE

Ahmad Kipande

Ahmad Kipande was born in Kilwa. In 1953 he decided to move to Dar es Salaam the capital city of  Tanganyika to look for employment. When he arrived in Dar es Salaam, among the things he found very interesting was gramophone technology, an instrument that could play the phonograph, and music could be heard.  78 rpm shellac records from Cuba were very popular. The titles were in Spanish, but they were also numbered beginning with the letters GV, they were famously known as the GV series records. Ahmad began to listen and enjoy the music from these great Cuban musicians, he also began to listen to music from East African musicians like Fundi Konde, Harry Makacha, and Frank Humplink and his sisters. Gradually, he began to have the desire to become a musician.

Kipande started teaching himself how to play various instruments by himself, in time he could play various instruments including the guitar, ukulele, banjo, and violin and finally he learned the saxophone, and this instrument brought him great fame. Ahmad’s first music group was the Tanganyika Jazz Band. Tanganyika Jazz Band was a group of individuals who formed the band as a hobby.  The band consisted of  guitars, violins, drums, trumpets and saxophones.

In 1958 Ahmad  decided to form his own band, and ​Kilwa Jazz Band was born. He bought all his instruments, none were electric, he then made his set of drums, at that time drums were made using tin barrels and cow or goat skin.

Among the first recruits of this band there was Zuberi Makata who was taught to play the sax by Kipande himself. Makata was knocked by a car and died later in his old age. The other recruits were Duncan Njilima and Omari Omari. At that time other bands that already existed in the city of Dar es Salaam and were trending were Homeboys Jazz band, Dar es Salaam Jazz band, and Cuban Marimba Branch Band, which was a branch of Cuban Marimba Band of Morogoro. The Morogoro Cuban Marimba band led by the late Salum Abdallah had many branches, for example, there was also the Cuban Marimba Branch of Kilosa.

Kilwa Jazz started playing music in various styles including rumba, samba, bolelo, and chacha.

Kilwa Jazz Band soon became one of the most popular bands in Dar es Salaam. Ahmad Kipande and his Kilwa Jazz Band participated in many national events. Kilwa Jazz Band was one of the groups that performed at the state house on 9th December 1961, the day Tanganyika got its Independence.  And they sang a special song praising Tanganyika for getting Uhuru. The song had these lyrics;

"O Lord, we ask you,

 Bless Tanganyika,

 We have got freedom

But hearts are sad,

Our comrades are suffering,

 The colonialists have still caught them in a web…”

 

 Kilwa Jazz Band was a very respected band, it was appointed by the government to participate in the Independence celebrations of Malawi and Uganda.

One of Kilwa Jazz most popular song was based on the words spoken by Mwalimu Nyerere 'It can be done, play your part'

Kilwa Jazz band had many songs that were loved and continue to be loved, among them there was a song called Kifo cha penzi. In short, the composer says, “The death of love is a bad thing, never pray for the death of love, and in the song we are reminded of two historical facts, one line says, 'It’s better to die by being hit by a double-decker bus going to Ilala', in those years there were double decker buses in Dar es Salaam . Another verse says 'It’s better to die by being hit by a trailer truck going to Zambia'. At the time cargo and oil to Zambia were being transported by trucks.

Mapenzi yananivunja mgongo (Love is breaking my back), Kifo cha pesa (Death of Money), Dolly, Nacheka cheka Kilwa leo (I am laughing today), Vijana tujenge nchi (Young people let's build our country), Rose wauwa (Rose you are killing me) are some of the songs from this band which was Ahmed Kipande's dream.

In 1973, Kilwa Jazz Band was invited to perform as a curtain raiser before the performance of the Rumba music legends, Franco and his T.P.OK Jazz at the National Stadium in Dar es Salaam.

Ahmed Kipande died on April 27, 1987, after suffering from a stroke for a long time, but he will continue to be remembered for the good music he left behind in this nation.

May Ahmad Kipande Rest in Eternal Peace.


Friday, August 19, 2022

IJUE HISTORIA FUPI YA DEKULA KAHANGA VUMBI


Dekula Kahanga Vumbi
 Kwa wapenzi wa muziki wa dansi Tanzania, jina la mpiga gitaa Dekula Kahanga Vumbi si geni, wengi hasa humfahamu kama mwanamuziki wa Maquis Original, na wanakumbuka mlio wa gitaa lake katika wimbo wa Ngalula, hasa pale ambapo Assossa anamhamasisha aongeze utamu kwa kutaja jina' Vumbi Vumbi'.
Lakini Je, mkali huyu alianzia wapi?
Kwanza kabisa  baba yake hakupenda kabisa apige gitaa,  lakini bahati nzuri alikulia kwa bibi yake katika mji wa Uvira, mkoa wa Kivu, Jamhuri ya Kongo. Kwa bibi kama walivyo wabibi wengi, alikuwa na uhuru zaidi na akaanza kwa kutengeneza magitaa yake, ambayo yalikuwa yakivunjwa kila baba yake alipokuwa akija kuwatembelea.

Jirani na alipokuwa akiishi kulikuweko na bar inaitwa Sikiya sosi ambapo palikuweko  na bendi ikiitwa Gramick Jazz, bendi iliyopitiwa na wanamuziki wengi ambao baadae walikuja Tanzania akiwemo Dr Remmy ngala. Vumbi alikuwa akisikiliza muziki ukipigwa ndani ya  hiyo bar na yeye akawa anafuatisha kwenye gitaa la kutengeza mwenyewe la nyuzi tatu, hatimae bibi yake akamnunulia gitaa dogo la nyuzi nne ambalo alikuwa anaenda nalo mpaka shule, ambapo mwalimu wake siku nyingine alikuwa akimwita awatumbuize wanafunzi wenzie.
Siku moja alikutana na jamaa aliyekuwa akipiga katika bendi iliyokuwa ikimilikiwa na mapadri, Dekula akawa anamnunulia sigara huyu jamaa nae akaanza kumfundisha chords mbalimbali za kupiga gitaa. Wanamuziki wengi wa zamani walipitia hatua hii ya kuwanunulia wakongwe sigara ili wafundishwe kupiga chombo. Mwanafunzi Dekula  aliendelea vizuri hatimae akajiunga na bendi hiyo ya mapadri iliyoitwa Kyalalo Band akiwa mpiga rhythm. Wanamuziki wa Kyalalo hawakuruhusiwa kujiunga na bendi zilizo kuwa zinapiga muziki kwenye bar, wala bendi yenyewe  haikuruhusiwa kwenda kupiga kwenye bar, kulikuweko na ukumbi mkubwa wa kanisa na hapo ndipo walipofanya mazoezi na maonyesho.  Hatimae Dekula aliiacha bendi hiyo ya mapadri na kujiunga na bendi Bavy National tena kama mpiga gitaa la rhythm.

 

Bavy National  Orchestre, kutoka kulia mstari wa nyuma ni Dekula (Rythm),Packot(Solo na Kiongozi),Maboko(Besi),
Merry-Djo (Drums).
Kutoka kulia mstari wa mbele,Waimbaji ni Djo-Mali,Issa Nundu na Simplice Mofeza.
Mwaka wa 1983  katika "Sikia Sosi Bar" Mjini  Uvira Mkoani Kivu Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Alipoingia Bavy National akakutana na mwimbaji Issa Nundu ambae alikuwa anafanya kazi hospitali, lakini jioni anajiunga na bendi, baada ya muda Kyanga Songa ambaye alikuwa Bwana Shamba nae alijiunga nao. Kyanga Songa  na Kasaloo Kyanga walipokuwa TANCUT Almasi Orchestra  Iringa, walinunua baiskeli na wakawa wanajiita Mabwana Shamba na baiskeli zao.
Katika kipindi hicho wakazi wa Kongo ya Mashariki, ambako kunazungumzwa Kiswahili, walikuwa wakisikiliza na kuzijua bendi nyingi kutoka Afrika ya Mashariki, bendi kama Tabora Jazz, Mangelepa, Simba wa Nyika, Mlimani Park zilisikilizwa sana maeneo hayo, na nyimbo kama Kassim ilikuwa moja ya nyimbo maarufu wakati huo na hivyo ikawa ndoto ya Vumbi na wenzie kuwa lazima siku moja waende huko unakotoka muziki mtamu huo ili nao waweze kushiriki. Katika kipindi hicho Kyanga Songa na Issa Nundu waliondoka  kwenye bendi yao ya Bavi National na kuelekea Tanzania, bendi ikatetereka sana, lakini kuondoka kwa hao wenzie kukamuongeza sana hamu Dekula ya kuja  Afrika Mashariki.
Siku moja mtu mmoja aliyeitwa Alida Shanga akamfwata Dekula na kumwambia kuwa ametumwa na Mzee John Luanda aliyekuwa anamiliki Chamwino Jazz Band, kuja kutafuta wanamuziki toka Kongo. Bila kusita Dekula na wenzie kadhaa wakafanya mipango na kuondoka Kongo kwenda Dar es Salaam Kujiunga na Chamwino Jazz band. Baada ya kushuka kwenye treni, kituo chao cha kwanza kilikuwa Tandale jijini Dar es Salaam, bila kuchelewa, siku waliofika na ndio siku wakaanza mazoezi.
Wakiwa bado vijana, yeye na wenzie watatu walikuja wakiwa na staili ya  kuimba na kucheza steji show ambayo wakati huo marehemu Julius Nyaisanga aliita sarakasi, si hivyo tu na pia wao ndio kilikuwa kikundi cha kwanza kuanza kurap katikati ya nyimbo. Waimbaji wakiwa ni   Sisko Lunanga, Fanfan Bwami, na mwenzao mmoja Baposta Kilosho ambae hatimae alirudi Kongo. 

Recording ya kwanza ilimuacha Julius Nyaisanga akishangaa vituko vya vijana hawa. Katika bendi ya Chamwino wakati huo wapiga magitaa walikuwa Vumbi Dekula, Kazembe wa Kazembe (huyu alikuwa Msukuma ambaye aliishi kwa muda Kongo na alikuwa mpiga gitaa hodari sana), na Mzee Albert huyu kwa sasa  yupo Manzese amepumzika. Baadae walimchukua Muhidin ambae alikuwa mpiga bezi wa Dr Remmy.
Siku moja walienda kuomba kupiga na Maquis Original, kwa ile staili ambayo wanamuziki huiita lift au kijiko,  wakati huo zaidi walikuwa wakipiga nyimbo za kopi kama Mario, Maze na kadhalika, hivyo wakazipiga hizo na watu wakafurahi sana na kuwatuza  fedha nyingi, wakachanganyikiwa maana bendi yao ya Chamwino ilikuwa haina mshahara na si mara moja walitembea kwa miguu kutoka Buguruni hadi Tandale kwa kukosa hata nauli.  Wakati huo kwa kuwa walikuwa wadogo kwa umri na hata umbo, marehemu Ndala Kasheba alikuwa akiwaita ‘Vimario’, hata hivyo upigaji wao ulikuwa mzuri sana.
Nguza aliwashauri wawe wanakuja kupiga kabla Maquis hawajaanza kupiga. Hivyo wakaamua kuiacha Chamwino, na wakawa wanasindikizana na Maquis, hili lilimuudhi John Luanda aliyewaleta nchini. Siku moja wakiwa Silent Inn, maafisa wa Uhamiaji walikuja kuwachukua wakalazwa Central Police na kisha kupelekwa gereza la Keko. Wakiwa huko walimwandikia barua Mzee Luanda kumuhakikishia kuwa watarudi Chamwino, basi wakaachiwa na kurudi na kuisuka upya Chamwino Jazz Band.
Lakini hawakukaa muda mrefu Mzee Makassy akaja kuwaomba waingie katika bendi yake, wenzake waimbaji  wakaenda  yeye akabaki Chamwino, lakini muda si mrefu Nguza akamwambia aandike barua ajiunge na Maquis. Nae akafanya hivyo na ndio kujiunga rasmi na Maquis kama mpiga gitaa la second solo. Aliwakuta wanamuziki kama Maneno Uvuruge, Omari Makuka, Keppy kiombile, Ilunga Lubaba, William Maselenge na wanamuziki wengine wengi wazuri.  Aliendelea kupiga second solo hadi siku moja bendi ilikuwa inapiga maeneo ya Ukonga, kwa kawaida Mzee Lubaba alikuwa anapiga kuanzia saa tatu mpaka saa sita, na  kisha Nguza Viking akiingia na kuendelea .

Maquis wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma,  wa pili toka kulia na shati jeusi Vumbi, wapili toka kushoto na suruali nyeusi Issa Nundu

Siku hiyo Nguza hakuonekana, Vumbi  akaweza kupiga nyimbo zote za Nguza, na kesho yake  akaambiwa afike ofisini akasainishwa rasmi mkataba wa kuwa mwanamuziki wa Maquis.  Baada ya muda mfupi Nguza akaacha bendi. Muda mfupi baada ya hapo walirekodi ule wimbo maarufu wa Makumbele, solo ya wimbo huu ilikuwa awali ikipigwa na Mzee Lubaba, lakini afya ya mzee Lubaba ilianza kuzorota nae akawa anawafundisha nyimbo zake wanamuziki wengine, wimbo wa Makumbele alifundishwa  Omari Makuka na akawa anaupiga katika maonyesho mbalimbali, lakini wakati wa kutaka kurekodi kamati ya uongozi ya Maquis iliamua Vumbi aufanyie mazoezi  na aurekodi. Kurekodiwa kwa album ya Makumbele ilitokana na safari ndefu ya bendi ambayo ilichukua miezi mitatu katika mikoa ya Ziwa, hivyo bendi iliporudi Dar  ilikuta sifa ya bendi imepungua, hivyo walirekodi album ya Makumbele iliyokuwa na nyimbo kama Tipwatipwa, Ngalula na Makumbele, sifa ya bendi ikarudi juu tena kwa mara nyingine. Na ni wakati huo ambapo bendi ilihamia katika ukumbi wa Lang’ata Kinondoni. Vumbi aliendelea kupiga katika bedi hii mpaka alipoamua kuhamia Sweden ambako yuko mpaka leo akiendelea kupiga muziki.

 



Thursday, August 18, 2022

TUMETIMIZA MIAKA 18 BILA PATRICK BALISIDYA

Patrick Balisidya, nyuma yake Salim Willis

Mwaka 1974 mwezi wa sita, ulikuwa mwezi wa furaha kwangu na wenzangu wa Operesheni Ukombozi pale Ruvu JKT.

Tulikuwa tumemaliza miezi sita ya kutumikia Jeshi la Kujenga Taifa ‘kwa mujibu wa sheria’. Mafunzo ya miezi sita yaliyoanzia kambi ya Mafuleta kule Handeni na kukakamilika katika kambi kubwa ya Ruvu, mkoa wa Pwani. Miezi sita iliyojaa visa na vituko  vingi vya ujana, marafiki wapya, na shughuli nyingi za kujenga ukakamavu,  kama vile mchakamchaka kila asubuhi, paredi, route march na mazoezi mbalimbali ya kivita na  kazi mbalimbali zikiwemo kilimo cha mpunga, ufugaji wa kuku na ng’ombe, hakika hakukuweko muda uliokosa shughuli. Hatimae siku ya mwisho ilifika tukafanya paredi kubwa ya kumaliza mafunzo, chini ya Mkuu wa Kambi Marehemu Meja Jenerali Rashid Makame. 

Baada ya paredi ya 'Pass Out', kulikuwa na shamra shamra nyingi za kumaliza mafunzo  zilizoishia na dansi lililoporomoshwa na bendi ya Afro 70.
Pamoja na kuwa nilikuwa nafahamu habari za bendi hii na pia nilishaanza kununua santuri zao toka mwaka 1973, siku hiyo ilikuwa siku ya kwanza kuiona bendi hiyo ikiwa jukwaani. Ilikuwa furaha juu ya furaha. Furaha ya kumaliza muda wa kulitumikia Jeshi la Kujenga Taifa juu yake furaha ya kuiona Afro70, bendi tuliyozowea kuiita Afrosa, kutokana na jina la mtindo wa muziki wake.
Dansi lilianza kama saa tatu usiku hivi baada ya chakula cha jioni, Afro 70 hawakutuangusha, na nyimbo zao zilizokuwa maarufu ziliporomoshwa usiku kucha, Dirishani, Weekend, Dada Rida, Pesa, Tausi na nyingine nyingi, pia bendi ilipiga nyimbo za wanamuziki waliopendwa miaka hiyo akina Clarence Carter, Otis Redding, James Brown, Aretha Franklin, ilikuwa raha kubwa. Sharti la muziki wa siku hii ya mwisho ilikuwa ni bendi kupiga muziki mpaka jua litakapochomoza kwani mabasi yalikuja mapema ili kuondoka na askari tuliokuwa tumemaliza muda kurudi makwetu. Alfajiri tulitoka kwenye muziki na masunduku yetu na kuingia kwenye mabasi kurudi makwetu.
Nimekumbuka sana siku hii kwa kuwa mwezi huu tunatimiza  miaka kumi na nane toka tulipo mzika Patrick Balisisdya, mtunzi, muimbaji, mpiga gitaa na kiongozi wa bendi ya Afro 70 pale makaburi ya Buguruni Malapa.

Patrick Pama Balisidya alizaliwa Mvumi Dodoma tarehe 18 April 1946. Mama yake alikuwa anapiga kinanda kanisani  hakika Patrick angeweza kujisifu kuwa muziki uko katika damu yake. Alianza kushiriki katika mambo ya muziki mapema na hata kuwa kiongozi wa Bendi ya shuleni kwake pale Dodoma secondary School. Alipomaliza shule ya sekondari akajiunga na Chuo cha Ufundi Dar es salaam, maarufu wakati huo kwa jina la Dar Technical, baada ya kumaliza mafunzo Dar Tech, alifanya kazi hiyo kwa muda na 1967 akawa tayari anapiga muziki Dar Es Salaam Jazz B.
Bendi hii ilikuwa inafanya kazi nzuri sana hivyo kuanza kuwa tishio kwa bendi kongwe Dar es Salaam Jazz Band yenyewe ( Majini wa bahari), na hivyo uongozi wa Dar Jazz ukaamua kuivunja bendi hiyo ndogo kabla haijaipoteza kabisa bendi kaka. Patrick hakufurahishwa na hatua hiyo, kufikia mwaka 1970 Patrick alikuwa ameanzisha kikosi chake mwenyewe kilichoitwa Afro70, kikiwa na mtindo wake Afrosa.
Mkongwe Shebby Mbotoni aliwahi nihadithia jinsi walivyokuja na wazo la kuanzisha bendi ya Afro 70, bendi iliyokuja kumtambulisha Patrick ulimwenguni. Shebby alisema siku moja alikuwa kwao akipiga gitaa, ndipo Patrick alipomkuta wakati akiwa anamtafuta rafiki yake aliyekuwa amepanga nyumba hiyo aliyokuwa akiishi Shebby. Basi alijitambulisha na wakaanza urafiki na ndipo likaja wazo la kuanzisha bendi,  na hatimae ikazaliwa Afro 70,
 Patrick alikuwa  mbunifu katika muziki wake, na kwa muda mrefu alikwepa sana kuingia katika wimbi la kufuata mapigo ya Kikongo kitu ambacho hata wakati huo bendi nyingi zilikifanya, hata bendi aliyokuwa akipigia, Dar es Salaam Jazz Band ilikuwa katika mkumbo huo wa kuiga bendi za Kikongo. Msimamo wa Patrick uliyumba baada ya kukutana na Franco wakati bendi ya TP OK Jazz ilipofanya ziara yake ya kwanza  nchini mwaka 1973, Patricka akaanza kuiga staili ya upigaji gitaa wa Franco. Wimbo wake wa Umoja wa kinamama, ulikuwa wazi umeiga sehemu kubwa wimbo wa Georgette wa TP OK Jazz.  

Afro70 ilipata bahati kuwakilisha wanamuziki wa Tanzania katika maonyesho ya mtu mweusi Lagos, Nigeria. (FESTAC festival 1977). Bahati hii ilikuja baada ya Afro 70 kushinda mashindano ya bendi yaliyoandaliwa na Wizara ya Utamaduni, kwa ajili ya kupata muwakilishi wa kwenda kwenye Tamasha hilo.  Baada ya mashindano, bendi ilipata fursa ya kuzunguka sehemu mbalimbali nchini kuonyesha kilichowafanya washinde na pia kupata mazoezi zaidi kabla ya safari ya kwenda Lagos. Lakini  bahati mbaya wakati wa kurudi Dar gari lao lilipata ajali na vyombo vya bendi vyote viliharibika. Wakati huohuo  Wizara ya Utamaduni ilikuwa imenunua vyombo vipya kwa ajili ya kuanzisha bendi yake, vyombo hivyo ilikabidhiwa Afro 70 kuvitumia FESTAC. Baada ya kurudi kutoka Nigeria Afro 70 waliamuliwa kurudisha vyombo vile serikalini, na  pia baada ya kurudi Festac bendi ilianza kusambaratika haikufanya onyesho tena kama Afro 70. Afro 70 ikafa rasmi.
Vyombo vile viliporudishwa serikalini vilitumika kuanzisha bendi ya Wizara ya Utamaduni iliyoitwa Asilia Jazz Band. Mwaka 1979, Balisidya alikwenda Sweden na kushirikiana na kikundi cha Archimedes akatoa album nzuri sana iliyoitwa Bado Kidogo. Patrick pia alipitia Orchestre Safari Sound, (Masantula) na kupiga piano katika ule wimbo maarufu, ‘Unambie siri’, alipitia pia bendi iliyoitwa Rainbow Connection, nakumbuka kukutana nae nilipotaka kujiunga na bendi hiyo wakati ikipiga pale New Africa Hotel, lakini Patrick akanishauri nisijiunge kwani alisema kuwa hakuwa anaona maendeleo yoyote katika bendi ile. Utabiri ambao ulikuja kuwa kweli bendi ilikuja kusambaratika.
Kwa kweli nyimbo za Patrick zilizokuwa juu katika chati ni nyingi,  Harusi, Dirishani, Weekend, Tausi, Pesa, Nakupenda kama Lulu, Ni mashaka na mahangaiko, Afrika, na nyinginezo nyingi. Patrick alifariki tarehe 7, Agosti 2004 na kuzikwa 12 Agosti katika makaburi ya Buguruni Malapa.

MUNGU AMLAZE PEMA PATRICK BALISDYA

 

KIKI, PROMO, PROPAGANDA, WATOTO WA BABA MMOJA

 


Kiki ni neno ambalo limekuwa maarufu zama hizi za Bongofleva. Kiki ni neno lilitokana na neno la Kiingereza, ‘kick’ yaani teke. Hivyo kiki maana yake katika ulimwengu wa wasanii ni kutafuta tukio ambalo litashtua jamii na kupaisha sifa yao au ya kazi yao. Ni kama vile ambavyo ukimpiga teke chura ndio unamsaidia kuruka. Hivyo wasanii wa zama hizi hutafuta kiki za aina mbalimbali ili kupaisha sifa za kazi zao, wengine hujitangaza kuwa wamefariki, wengine utakasikia wamefumaniwa, au wengine wameachana au wengine kutangaza wamerudiana au wameoana, au mara nyingine kueneza taarifa kuwa wimbo wao umeibiwa studio, na imefikia hata wazazi wa wasanii wengine kuingia kikamilifu katika shughuli za kiki kwa kutoa matamshi tata kuhusu kazi za watoto wao ili tu watu waelekeze masikio na macho yao kwenye kazi mpya. Pamoja na neno kiki kuwa jipya lakini hakika kutafuta kiki hakukuanza na Bongofleva. Makampuni yenye kutaka kutangaza bidhaa mpya sokoni, yamekuwa yakifanya matukio mengi makubwa kutafuta kiki. Makampuni hupitisha magari yenye maspika makubwa mitaani na kutangaza bidhaa zao, au hufanya matamasha makubwa, au huanzisha hata misemo tata ili tu kupata kiki ya bidhaa zao. Lakini hapa haiitwi kiki inaitwa promosheni. Wanasiasa nao hakika ni mabingwa wa kiki,wakati wa kutafuta kura, kila aina ya vituko hufanyika. Tumeshaona wanasiasa wanapiga magoti kuomba kura, wengine hata kugaragara chini wakiomba kura, hao wanaoamua kucheza ngoma za kiasili au dansi jukwaani ni kawaida sana.  Na wakifungua mdomo kueleza sifa walizonazo na watakachokifanya vyote ni kujinadi ili kuonekana bora, ila huku haiitwi kiki inaitwa siasa, au wengine huiita propaganda. Zama hizi hata viongozi wa dini nao wamo katika kutafuta kiki, utasikia wakishusha sifa za uwezo wao kama katika vyombo mbalimbali vya matangazo, wengine wamefikia mpaka kuingilia matatizo ya wasanii maarufu ili nao wajulikane kuwa wapo. Kutokana na malezi duni ya baadhi ya wasanii, kiki hizi zimekuwa zikichukua sura mpya siku hadi siku. Kwa sasa zimefikia hata kuongea, kutangaza au kuonyesha vitu vya faragha hadharani, ikiwa kama njia ya kutafuta kiki, na hapo ndipo ugomvi na watu wenye busara zao unapoanza.

Kama nilivyosema mwanzo neno kiki ni geni lakini shughuli zake si ngeni kabisa. Bendi za zamani zilikuwa na njia kuu moja tu ya kupata pesa nayo ilikuwa kwa  kiingilio mlangoni, gate collection, na hakika kulilazimika kuweko na mbinu za kujitangaza, au kutafuta kiki. Kulikuwa na njia kuu tatu za kutangaza onyesho,  kwanza ni kupitia redioni na pili kupitia magazeti, na tatu kwa kubandika matangazo kwenye kuta na nguzo za umeme. Magazeti yaliyokuwa yakishughulika na muziki yalikuwa ni magazeti ya serikali, magazeti ya Chama Cha Mapinduzi na magazeti ya chama cha wafanyakazi, NUTA na baadae JUWATA.  Vyombo hivi havikuwa na maadili ya kuruhusu ‘kiki’ za maisha binafsi ya wanamuziki, matangazo yalilazimika kuwa yanayohusu muziki tu.  Hivyo ubunifu ulikuweko, bendi zilijinadi kwa staili zake zenye mvuto ili kutafuta kiki. Kulikuweko staili kama  Katakata mwendo wa jongoo vumbi nyuma, Bomoa tutajenga kesho, Super mnyanyuo, Sikinde ngoma ya ukae, Mahepe ngoma ya wajanja, Dunda dunda, Bayankata, Kokakoka balaa  na majina mengine mengi. Matangazo kwenye magazeti yaliwekwa picha za wanamuziki au kuchorwa picha za kujinadi kwa njia moja au nyingine. Maswala ya kuachana, kupendana, kuhongana, kufumaniana hayakuhusika kabisa katika kutangaza kazi ya muziki. Nikifikiria sana nadhani vitu ambavyo wasanii wa sasa hufanya katika kutafuta kiki, vingefanywa na wasanii wa miaka ile na kutangazwa kama ilivyo sasa ingekuwa ndio mwisho wa msanii huyo, jamii ingemtema.

Nadhani moja ya sababu ya kuweko kwa kiki za ajabu katika zama hizi, ni kujaribu kujazia mapungufu yaliyomo kwenye sanaa husika. Msanii anakuwa anajua hata yeye kuwa kazi yake ni duni,  hivyo anazua kitu kisichohusika kabisa na kazi yake ya sanaa ili kuweza kuwafanya wateja japo wasikilize kazi yake kwa muda.

Taratibu za kurekodi siku hizi nazo zinafanya msanii asiwe na uhakika wa mpokeo ya wimbo wake hivyo kulazimisha vituko ili kujulikana kama ana kazi mpya. Msanii wa kizazi cha sasa anaweza kutunga wimbo asubuhi akaingia studio na kukamilisha wimbo na jioni wimbo uko tayari youtube na umeanza kurushwa kwenye vyombo ya utangazaji mbalimbali,

Hali haikuwa hivyo zamani, ukiwa na wazo la wimbo unalipeleka kwenye bendi yako yenye watu zaidi ya saba, wao wanakusikiliza na kuamua kama uchukuliwe na bendi au la, wakikubali ndipo mnaanza kuujenga wimbo, magitaa, ngoma. vyombo vya upulizaji, kila mtu anatoa wazo lake. Wimbo ulichukua japo siku mbili kukamilika, ingawa kuna nyimbo zilichukua hata zaidi ya wiki kuwa tayari. Bendi ikiridhika , wimbo ulianza kupigwa kwenye maonyesho, na hapa ndipo wapenzi wa bendi walikuwa wakiingia na kutoa maoni yao, mkikubaliana ndipo unaenda kurekodiwa. Mara nyingi bendi zilikuwa zinajua kabla hata ya kwenda kurekodi wimbo gani utakuwa maarufu kutokana na maoni ya wapenzi. Kwa taratibu hizo kiki za kujidhalilisha zilikuwa hazina nafasi, kazi ilikuwa inajiuza yenyewe.

Wednesday, August 17, 2022

SHAW HASSAN SHAW, MPIGA KINANDA ALIYEWAHI KUPANDA JUKWAANI AKAKUTA AMESAHAU KUPIGA NYIMBO ZOTE

Shaw Hassan Shaw
Kwa wapenzi wa nyimbo za Vijana Jazz Band hakika watakuwa wanakumbuka vile vipande vya kinanda vilivyokuwa vikianzisha zile nyimbo mbili alizokuwa akiimba Kida Waziri, Penzi Haligawanyiki na Shingo feni. Mpigaji wake alikuwa Shaw Hassan Shaw Rwamboh. Mwanamuziki huyu alizaliwa tarehe 25 September 1959, Dar Es Salaam. Alianza kujifunza kupiga gitaa na wenzie kando ya Ziwa Tanganyika huko Kigoma, wakitumia magitaa ya tajiri mmoja aliyekuwa na meli ya uvuvi. Alipokuja Dar es Salaam akakutana na mwanamuziki Zahir Ally Zorro, Zahir ndiye aliyeboresha upigaji wake wa gitaa kiasi cha kukubaliwa na Patrick Balisidya kupiga gitaa la rythm katika bendi yake ya pili PAMA Band, chini ya Afro70.

Shaw Hassan Shaw wa kwanza kulia aliyenyoosha mkono. Mwendeshaji wa blog hii John Kitime wa kwanza aliyesimama kushoto. Hapa wakiwa Stadium Morogoro wakingojea onyesho la kumkaribisha Nelson Mandela.

Ni chini ya malezi ya Patrick alipojifunza kupiga Keybords (Kinanda). Baada ya hapo aliacha muziki na kujiunga na Dar Technical College. Lakini 1980 alijiunga na Vijana Jazz kama mpiga Keyboards, alishirikiana na wanamuziki wengi lakini wengi kwa mapenzi ya Mungu,  wametangulia mbele ya haki. Baadhi ya waliobaki kati ya aliyokuwa nao wakati huo ni John Kitime, Kida Waziri, Saad Ally Mnara, Hamisi Milambo, Huluka Uvuruge, Hassan Dalali, Hamza Kalala na Rashid Pembe. Mwaka 1990 alijiunga na Orchestra Safari Sound, chini ya Maalim Muhidin Gurumo (MJOMBA) na Marehemu Abel Baltazar, hapa alikutana na akina Benno Villa Anthony na Mhina Panduka (Toto Tundu) .Aliacha bendi baada ya miezi sita tu, mwenyewe anasema, ‘….kutokana na muhusika kutozingatia mkataba wangu…’. Alihamia Zanzibar na kujiunga na bendi iliyokuwa ikipiga Mawimbini Hotel, hakukaa sana kwani Washirika Tanzania Stars walimwita. Hapa akakutana na mwalimu wake wa gitaa Zahir Ally, Ally Choki, Musemba wa Minyugu,Tofi Mvambe, Abdul Salvador na wengine, ilitokea kutoelewana baina ya wanamuziki na yeye kama kiongozi wa bendi ilibidi aachie ngazi kuepusha bendi kuzidi kujichanganya. Baada ya hapo Kanku Kelly ambaye ni mume wa dada wa mke wake alimuita ajiunge na Kilimanjaro Connection Band. Anasema Kanku alimvumilia sana kwa kuwa alikuwa hajawahi kufanya kazi ya kukopi nyimbo za wanamuziki wengine wakubwa duniani, hatimae akaweza kujiendeleza na kuweza kumudu kupiga vitu vikubwa, bendi hii ya Kanku  ilikua inazunguka kwa kupiga muziki hotel mbalimbali katika nchi za Malaysia, Singapore, Indonesia, Thailand na Japan jambo ambalo lilifanya aone kila kitu ni kigeni kila alipokwenda. Katika bendi hiyo alishirikiana na akina Kanku Kelly, Mafumu Bilal, Maneno Uvuruge, Burhan Adinan, Shomari Fabrice, Bob Sija, Fally Mbutu, Raysure boy, Delphin Mununga na Kinguti System. Baadaye Shaw, Kinguti na Burhan Muba waliamua kuanzisha kundi dogo wakitumia sequencer keyboards na kumuaga Kanku Kelly. Group hili lilijiita Jambo Survivors Band, bendi ambayo itakumbukwa  kwa ule wimbo Maprosoo ulioimbwa na MlasiFeruzi ambao uliokuwa katika album ya MAPROSOO.
Mlasi feruzi
Baada ya hapo bendi ikaanza kuzunguka nchi mbalimbali ikipiga katika mahotelini. Kupitia muziki Shawa amekwisha fika Oman , Fujairah, U.A.E, Singapore, Malaysia na Thailand. Shaw anasema wanamuziki ambao hatawasahau kwa kuwa wamemfikisha alipo ni Zahir Ally Zorro, Marehem Patrick Balisdya, Waziri Ally, Kinguti System, Burhan Muba na Kanku Kelly. Kituko ambacho hawezi kusahau ni nchini Malasyia wakati akiwa na Kanku Kelly na ikiwa ni mara ya kwanza kwake kupiga muziki akiwa amezungukwa na watu weupe watupu. Anasema nyimbo zote zilipotea kichwani akawa hakumbuki hata nyimbo moja aliyokuwa kafanyia mazoezi

MJUE JEAN 'JOHNNY' BOKELO ISENGE

 

 


 Jean ‘Johnny’ Bokelo Isenge alizaliwa mwaka 1939 nchini Kongo, nje kidogo ya jiji la Kinshasa. Familia yake ilikuwa ni ya wanamuziki. Johnny alikuwa mdogo wa Paul Ebengo’Dewayon’ Isenge mwanamuziki mwingine aliyekuwa mkubwa sana nchini Kongo toka mwanzoni mwa miaka ya 50. Huyu Dewayon alikuwa na bendi inaitwa Watam, hapa ndipo Johnny alipoanzia muziki akipiga na mtoto mwingine aliyekuja kutikisa ulimwengu wa muziki Franco Luambo Luanzo, wakati huo Franco akiwa na miaka 12 tu. Johnny Bokelo aliendelea kupiga katika bendi alizoanzisha kaka yake kama vile Conga Jazz na Orchèstre Cobantu, lakini mwaka 1958 Johhn akaanzisha bendi yake, Orchestre Conga Succès, akiwa na mdogo wake Mpia Mongongo maarufu kwa jina la Porthos Bokelo, ambaye alikuwa mpiga gitaa la rhythm mahiri sana. Kaka yao Dewayon, akaja kujiunga na kundi hilo1960 lakini miaka miwili baadae1962 Johnny na kaka yake wakatengana. Bokelo alifanikiwa kulijenga kundi lake kuwa na nguvu na likawa kwa namna fulani linafanana sana na OK Jazz. Hata tungo nyingine zilikuwa ni za kujibu tungo za OK Jazz au kuzungumzia mada ambayo imeanzishwa na OK Jazz. Hii haikuwa kwa ugomvi bali kutokana na ukaribu uliokuwa kati ya Franco na Johnny. Kuna wakati Bokelo alianzisha mtindo wa kutunga nyimbo alizozipa jina la Mwambe, kukawa na Mwambe no 1 na 2 mpaka 5 ambapo alikuwa akiongea na kushangaa jamii inaelekea wapi. Upigaji wa Bokelo Dewayon na Franco ulishabihiana, pengine ni kutokana na wote kuanzia Watam. Mwaka 1968 Johnny Bokelo akabadili jina la kundi lake la Conga succès” na kulita “Conga 68” akaanzisha label yake akaanza kutoa santuri, hii ilimuongezea kipato japo wanamuziki wake walitishia kuachana nae kwani walisema hawakuwa wanapata fedha zozote kutokana na mradi huo. Santuri nyingi wakati huu alikuwa akiziachia kwanza kutoka Ufaransa ili kupata mapato zaidi. Kati ya 1972 mpaka 1974 Bokelo Isengo alikuwa anatumia muda mwingi zaidi akiwa studio, kwenye mwaka 1970, viwanda vya kutengeneza santuri vya Kinshasa vikawa vimechoka hivyo bokelo akaanza kupeleka master zake Kenya ili kutengeneza santuri. Mwaka 1980 Bokelo aliachana sana na shughuli za muziki.

Bokelo alifariki 15 January 1995 baada ya kuugua kwa muda mrefu

 

 



Friday, August 12, 2022

HAKIKA DANSI LIMEBADILIKA SANA

 


Kweli dansi limebadilika sana.

Kumbukumbu zangu huwa zinanirudisha Iringa nilipokuwa na umri wa miaka minne hivi. Nadhani ndipo nilipoanza kutambua kuwa wazazi wangu walikuwa wanajitayarisha kwenda dansini, nakumbuka wakituaga na kutumbuambia ‘Haya laleni sisi tunaenda dansini’. Moja ya dansi nakumbuka lilikuwa limepigwa na Cuban Marimba wakiongozwa na Salum Abdallah, nakumbuka kwa sababu kesho yake Mwalimu Nyerere alikuja kuhutubia kwenye uwanja ambapo upo sasa ni uwanja wa Samora. Wakati huo ulikuwa ni uwanja wa mpira wa shule ya Middle School na baba yangu alikuwa Headmaster wa shule ile, na nyumba yetu ilikuwa pembeni tu ya uwanja huo wa mpira.
Siku alipokuja kuhutubia Mwalimu Nyerere, wimbo uliokuwa ukisikika kwenye spika ukirudia rudia, ulikuwa wimbo wa Cuban Marimba na baadhi ya  maneno yake yalikuwa ‘ Tutie jembe mpini, twendeni tukalime’. Mama akatuambia na wadogo zangu kuwa wimbo huo walikuwa wameucheza jana yake dansini. Kwa kweli toka nikiwa mtoto, dansi kwangu ni neno la furaha  kwenye maisha yangu. Nikiwa mdogo  wazazi wangu walikuwa wakituonyesha namna ya kucheza aina mbalimbali za dansi, zikiwemo tap dancing, aina ya dansi ambayo viatu lazima uvigonge sakafuni wakati wa kucheza kufuatia mapigo ya muziki, wazazi walitufundisha kucheza  chacha, waltz na aina nyingine za dansi ambazo sijapata hata  kujua majina yake.
Nyakati hizo na miaka mingi baadae, mtu akiaga anakwenda dansini, jambo la muhimu atakalolifanya huko ni kucheza nyimbo nyingi kadri atavyoweza. Kesho yake mazungumzo kuhusu dansini ni kuulizana nyimbo ngapi zilichezesha. Mpenzi wa muziki kurudi nyumbani akiwa kachoka kwa kucheza ilikuwa ndio dalili ya kufurahia kwa usiku ule.

Miaka mingi baadae hatimae nikaja kuwa mwanamuziki wa muziki wa bendi,  aina ya muziki ambao miaka ya 80 ulianza kuitwa muziki wa dansi, ulipewa jina hili kuutofautisha na aina nyingine za muziki kama vile taarab,  kwaya, muziki wa asili na aina nyingine za muziki. Muziki huu wa dansi ulikuwa ni ule uliopigwa kwa vifaa vya kisasa na kutegemea kuwa lazima utachezwa, tena kwa mtindo maalumu.  
Katika miaka ya hamsini na mwanzoni mwa miaka ya sitini, bendi zilikuwa zikitangaza aina muziki itakaoupiga, kwa mfano kiongozi wa bendi aliweza kutoa maelezo yafuatayo kabla ya kupiga wimbo. ‘ Muziki ufuatao unaitwa Dada Adija, umepigwa katika mtindo wa Cha Cha’. Basi muziki ukianza wapenzi wa muziki huingia uwanjani na kuonyesha umahiri wao wa kucheza ChaCha. Na hivyo hivyo kama wimbo ni Twist, Bolelo, Charanga na kadhalika. 

Utunzi wa zamani

Utunzi wa nyimbo mpya za bendi ulikamilishwa kwa muungano wa mawazo kutoka kwa wanamuziki mbalimbali katika bendi. Mtunzi wa awali aliweza kuleta  mashahiri, mara nyingine yakiambatana na melodia na kuwaimbia wenzie ambao kama wangeukubali, walianza kutunga vipande mbalimbali vya wimbo kupitia  vyombo mbalimbali wanavyovipiga. Tungo nyingi za awali zilianza kwa rumba, na ilipofika katikati mwendo ulibadilika na kuingia katika kile tulichokuwa tukikiita ‘chemka’.
 Chemka mara nyingi ilianza kwa kuimba na kisha kuingia kipande cha gitaa la solo. Hapa ndipo wapiga solo walikuwa wakipimwa kwa umahiri wao wa kutunga na kupiga vipande vya solo ambavyo vingeweza kuwateka akili wasikilizaji na kuwafanya wacheze dansi.
Katika bendi nilizopitia kama vile TANCUT Almasi na Vijana Jazz Band, baada ya bendi kukamilisha wimbo, ulianza kupigwa katika maonyesho mbalimbali, lakini jambo la muhimu ambalo wanamuziki wote tulikuwa tunaliangalia lilikuwa Je, watu wanaucheza wimbo mpya? Ikionekana wimbo  umekosa hamasa ya kuwasimamisha  wachezaji, wimbo huo ulirudishwa mazoezini na kubadilisha vitu tulivyohisi vinafanya watu wasipende kucheza wimbo ule. Na mara nyingine wimbo huo ulitupwa pembeni moja kwa moja kama haukuchezesha, mamia ya nyimbo  katika bendi mbalimbali ziliishia kupigwa kwenye kumbi mara moja tu na hazikurudiwa tena, kwa kuwa tu watu hawakuchangan mkia kuzicheza.
Siku hizi mambo yako tofauti kabisa, unaweza kuingia kwenye onyesho la muziki wa Taarab, muziki ambao kwa asili ulikuwa ukisifika kwa kuwa muziki wa kusikiliza tu, ukakuta wapenzi wakitiririka jasho kwa kucheza nyimbo mbalimbali za Taarab, halafu ukaingia katika onyesho la ‘muziki wa dansi’, ukakuta waimbaji wakitoka mishipa ya shingo lakini hakuna anaeshughulika kucheza dansi hilo. Kama ingekuwa  zamani, hiyo ni dalili ya moja kwa moja kuwa muziki huo hauwafurahishi wapenzi. Lakini hizi ni zama nyingine.

Katika zama hizi, bendi huwa na wacheza show wake au hata waimbaji nao wakatengeneza show, kisha wakawa wanapiga muziki na kucheza wao wenyewe. Sijui nilinganisha na kujitekenya halafu kucheka mwenyewe?
Teknolojia imeleta aina nyingine ya kuonyesha upenzi na unazi wa muziki. Wapenzi wa muziki siku hizi huonyesha upenzi wao wa muziki kwa kuchukua simu na kurekodi video za  bendi zikiimba na kucheza, wao wenyewe wakiwa wamekaa kwenye viti wakiendelea kunywa vinywaji vyao, kisha vipande hivi vya video husambazwa kwenye makundi ya Whatsapp, vikiambatana na sifa kuhusu ubora wa bendi hizi. Ndio namna ya ‘ku appreciate’ muziki zama hizi.
Lakini pia kuna madansi ambayo utakuta wapenzi wamechangamka wanacheza sana, lakini ukiangalia kila mtu anacheza akili inavyomtuma, hakuna tena mpangilio wa kucheza staili maalumu ya muziki. Ile staili ya wapenzi kukumbatiana kwa hisia wakati wa kucheza rumba imepotea, si ajabu kabisa kumkuta mtu na mpenzi wake wanacheza wimbo wa taratibu, lakini kila mtu na staili yake na juu ya hayo kila mmoja anatuma meseji kwenye simu yake.
Hakika dansi limebadilika sana

 

Wednesday, August 10, 2022

WANAMUZIKI WA SASA WANAKUBALI KUKOSOLEWA?

 

Top Ten Show 1989

Jana nilikuwa naangalia maktaba yangu ya kanda za video za zamani, nikaiona kanda moja iliyonirudisha miaka mingi sana nyuma. Ilikuwa ni kanda ya video ya onyesho moja la bendi ya Tancut Almasi Orchestra lililofanyika katika ukumbi wa klabu ya bendi hiyo eneo la Sabasaba pale Iringa.
Mwaka 1989 yalianza kufanyika mashindano ya bendi yaliyoitwa Top Ten Show, mashindano haya yalifikia kilele mwaka 1990. Yalikuwa ni mashindano makubwa sana ya muziki wa dansi na mpaka leo hayajawahi kufanyika mashindano ya bendi yenye ukubwa ule. Mashindano haya yaliyotayarishwa kwa ushirikiano wa CHAMUDATA, Radio Tanzania na Umoja wa Vijana wa CCM, yalianza tarehe 29 Julai 1989 na kufikia kilele tarehe 25 November 1989. Bendi zilizoshiriki zilikuwa 50 kutoka mikoa ya Dar es Salaam, Arusha , Kilimanjaro, Tanga, Iringa,  Mbeya,  Morogoro, Rukwa , Kigoma na Pwani. Hii ilikuwa maendeleo kwani Top Ten Show ya mwaka 1988 ilikuwa na bendi 27 tu. Wafanyakazi wa Radio Tanzania Dar es Salaam  walizunguka katika mikoa mbalimbali na bendi za huko zilifanya maonyesho ambayo yaliyorushwa ‘live’  redioni na hivyo kuwapa wasikilizaji nchi nzima nafasi ya kusikiliza na kufuatilia mashindano hayo katika hatua zote.  Mwaka huo nilishiriki mashindano haya wakati nikiwa mmoja wa wanamuziki wa bendi ya TANCUT Almasi Orchestra iliyokuwa na masikani yake mjini Iringa.  Masharti ya mashindano tulipewa mapema sana. Kila bendi ilitakiwa ijitayarishe kwa nyimbo tatu, mmoja uwe unaitwa Nakulilia Afrika, wimbo wa pili ulikuwa lazima utokane na wimbo wa tuni ya asili ya kabila mojawapo la Tanzania na wimbo wa tatu uwe wimbo wowote ambao bendi ilipendelea kuupiga. Tulianza kufanya mazoezi makali  ya nyimbo hizo. Marehemu Kasaloo Kyanga na pacha wake Kyanga Songa wakaja na tungo yao ya wimbo Afrika Nakulilia, na mimi nikatoa mchango wa wimbo wa asili ya Kihehe ulioitwa Lung’ulye, kwa pamoja tukaamua kuwa wimbo wetu wa tatu uwe Ngoma za Afrika uliokuwa utunzi wa Kalala Mbwebwe.
Baada ya mazoezi makali tuliamua kufanya onyesho lisilo la kiingilio na kuwakaribisha wapenzi wa muziki wa dansi pale Iringa kuja kutoa maoni yao kuhusu matayarisho yetu hayo.  Mkuu wa Mkoa wa Iringa wakati huo, Mama Mary Chipungahelo alikuwa mgeni rasmi  wa onyesho hilo. Kilichofanyika pale siku ile, kilikuwa si kitu ambacho naona kitawezekana kwa urahisi katika zama hizi. Baada ya kupiga nyimbo zile wapenzi walikaribishwa jukwaani  kuongea ukweli kuhusu nyimbo zile, tuliomba waliotaka kutoa sifa wakae nazo, tulichokuwa nania nacho ni mapungufu katika matayarisho hayo. Hakika kulikuweko maneno makali ambayo sidhani wasanii wengi siku hizi wangekubali kukosolewa vile. Kulikuwa na kukosoa kuanzia mavazi, uchezaji na hata tungo zenyewe. Tungo ya Afrika Nakulilia iliyotungwa na akina Kasaloo ilikataliwa kwani ilionekana ilitokana na wimbo wa Pepe Kalle, hivyo muimbaji Kalala Mbwebwe na mpiga gitaa la solo Kawele Mutimwana wakaleta tungo nyingine ambayo ndio ilikuwa moja ya kete zetu katika mashindano yale.



Baada ya kuvuka kigingi cha wapenzi wetu wa Iringa, tulikuja Dar es Salaam na tulikuwa tumepangiwa katika kituo cha ukumbi wa Silent Inn uliokuwa eneo la Mpakani Dar es Salaam. Katika onyesho hilo, tulikuwa jukwaani pamoja na bendi iliyokuwa ikiitwa Orchestra Linga Linga Stars wakati huo muimbaji wake mahiri alikuwa Karama Regesu ambaye kwa sasa yupo Msondo Music Band. Tancut tukaibuka kuwa katika bendi kumi bora na kuja kushiriki fainali za onyesho lile zilizofanyika uwanja wa Taifa. 
Baadhi ya bendi zilifika kumi bora  zilikuwa, Tancut Almasi, Super Matimila, MK Group, Salna Brothers, Varda Arts, Bima Lee, Kilimanjaro Band na Vijana Jazz Band, hakika Uwanja wa Taifa palipendeza siku ile. Lakini kwangu mimi mambo yalikuwa na utata kidogo kwani siku ya fainali, nilikuwa nimeshamia Vijana Jazz Band, lakini kwa siku hiyo nilirudi bendi yangu ya zamani ya  Tancut Almasi  kwani wakati wa mashindano nilishiriki katika bendi hiyo. Uwanja wa Taifa ulijaa wanamuziki wengi sana, na kwa kuwa bendi zilikuwa na ustaarabu wa kuvaa sare, basi sare za aina mbalimbali zilitawala siku hiyo.

Ushindi wa TANCUT

 Hatimae matokeo yalitangazwa na kila wimbo ulikuwa na mshindi wa kwanza mpaka wa kumi, washindi watatu wa kwanza wakipata zawadi mbalimbali. Wimbo wangu wa asili ya Kihehe, ulishinda zawadi ya kwanza katika nyimbo za kiasili na washiriki wote tulipewa ‘radio cassette’ zilizotolewa na Ubalozi wa Uholanzi. Wimbo Afrika Nakulilia ulishika nafasi ya pili na wimbo uliokuwa chaguo la bendi ulikuwa Ngoma za Kwetu uliokuwa utunzi wa Kalala Mbwebwe ulichukua nafasi ya nne katika kundi lake, Kwa ujumla matokeo yalikuwa mazuri sana kwa bendi ya TANCUT Almasi.
Wanamuziki na viongozi wa TANCUT ALMASI Orchestra wakiwa na zawadi zao


 Art Critic

Katika nchi ambazo sanaa imekuwa, huwa kuna watu wanaoitwa ‘art critics’, hawa kwa kweli ni mabingwa katika fani za sanaa wanazo shughulikia na wao kazi yao moja kubwa ni kukosoa kazi mbalimbali za sanaa na hatimae hata kuzipa grade. Kwa mtizamo wa haraka haraka utaweza kudhani kuwa kukosoa kwao kunaweza kuharibu soko la sanaa husika, lakini kwa kuwa hawa watu huwa wakweli na wenye uzoefu, wasanii huwa wanafuatia sana watu hawa wanasemaje kuhusu kazi zao. Kupasishwa na watu hawa hupandisha thamani ya sanaa husika. Wakosoaji hawa pia huwafanya wasanii wawe makini katika kazi zao na hivyo ubora wa sanaa nzima unapanda.  Kitendo cha bendi ya TANCUT kuruhusu kukosolewa kabla ya kuingia katika mashindano ilikuwa sababu moja wapo ya bendi kupata ushindi mnono katika mashindano yale. Wasanii wa sasa hapa nchini wako tayari kukosolewa?

Friday, August 5, 2022

TUZIKUMBUKE BENDI ZETU ARUSHA NA MOSHI

 

The Ambassador Band ya AICC

Safari ya kuzikumbuka bendi zetu leo inatufikisha miji ya kaskazini mwa nchi yetu. Jiji la Moshi na jiji la Arusha. 
Tuanze na jiji la Moshi, hakika  ukisikiliza hadithi mtaani za siku hizi unaweza ukadhani Moshi si mji wa kuwepo katika historia ya muziki, lakini kinyume kabisa, huwezi kuongelea historia ya muziki Tanzania bila kutaja Moshi. Kwanza kuna mchango mkubwa wa wanamuziki waliotoka Moshi, na pili kati ya wawekezaji wakubwa katika muziki waliowahi kutokea Tanzania, waliotoka Moshi.
Taja bendi karibu zote zilizokuwa kubwa miaka ya sitini na sabini utaukuta mkono wa muwekezaji toka Moshi.
Wanamuziki wa Moshi walianza kuiweka Tanzania katika ramani ya muziki wa Afrika ya Mashariki kuanzia miaka ya 50. Mabingwa kama Frank Humplick na Dada zake, ambao walikuwa watoto wa  baba muhandisi kutoka Austria na mama Mchaga,  Dr Hosea Macha na mke wake, Dr Hosea alikuwa baba mzazi wa mwandishi na msanii maarufu Freddy Macha,  Kimambo Brothers na wengine wengi waliweza kurekodi nyimbo zao kwa mtindo ule wa kutumia gitaa kavu, yaani gitaa lisilotumia umeme. Frank Humplick alirekodi nyimbo nyingi na wasanii wa Kenya chini ya lebo ya Jambo, ukiwemo wimbo maarufu Mi Francois mi naimba,ambao alifanya ‘kolabo’ na mwanamuziki kutoka Kongo Edward Mazengo, mambo yote hayo kabla ya Uhuru.
Baadhi ya bendi nyingine  zilizokuweko Moshi ni Ringo Jazz, halafu kulikuweko na Black Beatles, hawa walikuwa wakivaa kama wale wanamuziki wa Beatles wa Uingereza, walikuwa na gari lao la Combi ambalo waliliandika maandishi makubwa Black Beatles.  Moshi pia ilikuweko bendi maarufu ya Zaire Success, hii ilikuwa bendi ya vijana wa Kikongo. Kulikuwa na hadithi zamani ikisema hawa walikuwa ni kundi lililovunjika kutoka kutoka kwa kundi la Orchestra Fauvette la akina King Kiki na Ndala Kasheba Supreme, hata lile kundi la bendi ya Wakongo la Mwanza lilioitwa Orchestra Super Veya nayo husemekana ilitokana na mpasuko wa Orchestre Fauvette.
Mara ya mwisho kuingia muziki wa Zaire Success ilikuwa mwaka 1974 walipopiga community center Same, siku ilipofunguliwa Benki ya kwanza mji huo. Mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Bwana Peter Kisumo. Mimi na rafiki zangu tulizuiliwa kuingia kwa kuwa kulikuwa na mgambo mlangoni kazi yake ilikuwa kuangalia waliovaa nguo zisizofaa,  tulikuwa tumevaa suruali zetu zilizokuwa pana chini, maarufu kwa jina la bugaluu. Ikalazimu kwenda kubadili ili kuweza kuingia dansi lile.  Nigusie hapa kuwa kuwa Same pia kulikuwa na bendi iliyoitwa TANU Youth League Jazz Band, kuna Askofu maarufu alikuwa mwanamuziki wa bendi hiyo miaka hiyo ya 70.

Chuo cha Polisi cha Moshi maarufu kwama Police Training School, PTS, kwa miaka mingi ilikuwa na bendi moja nzuri iliyokuwa ikitumbuiza mjini Moshi mara kwa mara. Moshi pia kulikuwa na bendi iliyokuwa inaitwa Bana Afrika Kituli, awali ilikuwa bendi kubwa ikaapoteza umaarufu mpaka ikawa inapiga kwenye vilabu vya mbege. Mmoja wa wanamuziki wa bendi hii niliwahi kumkuta Tanga akiwa amebadili taaluma na kuwa mganga wa kienyeji. Ni jambo la ajabu kidogo lakini kuna wanamuziki wengi sana ambao walikuja kuacha muziki na mkuwa waganga wa kienyeji.
Shule ya sekondari ya Old Moshi na hata Shule ya Ufundi ya Moshi ( Moshi Tech), zote zilikuwa na bendi ambazo zilikuwa zikipiga muziki kwa umahiri wa hali ya juu. Bendi ya shule ya Old Moshi walijiita Orchestra Mosesco. Baadhi ya wanamuziki wa bendi hii walikuwa Joseph Mkwawa, Pelegrin, Mwakibete, Tamba, Kufakunoga  na kadhalika.
Tuhamie Arusha, mji ambao katika miaka ya mwanzo ya sabini ulikuwa umechangamka sana kutokana na kuwa na wafanyakazi wengi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, halafu ukijumlisha na  biashara ya utalii, hakika mji ulikuwa na burudani nyingi. Hoteli za kitalii zilizokuwa chini ya Shirika la utalii Tanzania, karibu zote zilikuwa zikishindana kuwa na bendi bora hotelini, bendi kama The Revolutions, ambayo baade iliitwa Kilimanjaro Band, The Bar Keys ambayo ikaja kuitwa Tanzanites ni baadhi ya bendi ambazo zilitamba sana kwenye mahoteli ya Arusha. Bendi chache nyingine zilizokuwa zikipiga mahotelini ni Juju Masai ya akina Sabuni, hawa walikuwa ndugu waliokuwa mahiri sana katika muziki,  Crimson Rage, Ambassadors akina Andy Swebe na Likisi matola (wanaoonekana pichani), Tonics ya David Marama  na kadhalika.

Kwenye uwanja wa muziki wa Rumba kulikuwa na bendi kama Orchestra National, bendi ambayo ndio aliyoanzia muimbaji mahiri sana Hassan Bitchuka kabla ya kuonekana na NUTA Jazz Band. Kulikuwana Arusha Jazz Band, bendi iliyokuwa ya akina Wilson Peter na wenzie baada ya kuihama Jamhuri Jazz Band ya Tanga. Arusha Jazz Band ilihamia Mombasa na ndipo ikabadili jina na kujiita Simba wa Nyika, umaarufu wa bendi hiyo unafahamika kwa wapenzi wote wa muziki wa zamani. Arusha pia kulikuwa na bendi ya Chuo Cha Jeshi Monduli, bendi iliyoitwa Les Mwenge, bendi iliyokuja kupata umaarufu mkubwa kutokana na album ya wimbo Kila munu ave na kwao wa Halila Tongolanga.

Ukurugenzi wa Mkoa wa Arusha  ulianzisha bendi, nadhani ulikuwa ukurugenzi wa kwanza kufanya hivyo baadae mikoa mingine ikafuatisha. Bendi hiyo  iliundwa na  wanamuziki wa bendi ya Orchestra Lombelombe, bendi iliyokuwa ni matokeo ya mpasuko wa Morogoro Jazz band. Bendi hiyo mpya ikaitwa Kurugenzi Arusha. Kurugenzi Arusha ilitunga nyimbo kadhaa zilizotikisa anga ya muziki nchini, nyimbo  kama vile Wivu na Ujamaa mpaka leo bado zina wapenzi lukuki. Mwisho huwezi kuongelea bendi za Arusha bila kuitaja  Serengeti Band, bendi iliyoanzishwa na mmoja ya wanamuziki wa Orchestra Mkwawa iliyokuwa bendi ya shule ya Mkwawa, mwandishi mkongwe Danford Mpumilwa, hakika bendi hii nayo ilichangamsha jiji la Arusha.

Thursday, July 28, 2022

TUZIKUMBUKE BENDI ZETU 6 -MBEYA

 


Hebu tuendelee na safari ya kukumbuka bendi mbalimbali nchini, leo tuanzie mkoa wa Mbeya, tuanze na wilaya ya Mbeya, wilaya ambayo kabla ya mwaka 1927 ilikuwa ikijulikana kama wilaya ya Igali.
Mbeya ilikuja kuanza kupata umaarufu kutokana na kugundulika kwa dhahabu sehemu mbalimbali za kuzungukia mji huu kuanzia mwaka1906, hali iliyoendelea kwa karibu miaka ishirini baada ya hapo. Mji ukapata wageni kutoka kila kona ya Afrika Mashariki na Kati mpaka visiwa vya Ngazija, watu wakaja Mbeya na miji jirani kutafuta utajiri.

Popote penye vijana wengi, tena wakiwa wanatafuta pesa, hakukosekani burudani na hasa burudani ya muziki. Bahati mbaya si mengi yaliyohusu burudani za wakati huo yaliyowekwa kwenye kumbukumbu,lakini kati ya machache tuanze na historia ya mtu moja aliyekuwa maarufu sana aliyeitwa John Benedict Mugogo Mwakangale, mwenyewe alipendelea kuitwa JBM. John Mwakangale, JBM alikuwa mwanasiasa mashuhuri katika harakati za kupigania Uhuru na baadae katika siasa ya kutafuta umoja wa Afrika. Alifanya kazi kubwa ya kutambuliwa na hatimae alikuweko katika Baraza la Mawaziri la kwanza la Tanganyika huru chini ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, na akateuliwa kuwa Waziri wa kwanza wa Kazi, pia alikuwa Mbunge wa Nyanda za juu kusini kwa kipindi kirefu, kabla ya Uhuru na hata baada ya Uhuru. Pamoja na yote hayo JBM pia alikuwa mpenzi mkubwa wa muziki. Kati ya mwaka 1959 na mwaka 1960 alikwenda Zambia, wakati huo ikiitwa Northern Rhodesia, alikwenda kununua vyombo vya muziki kwa ajili ya bendi yake iliyoitwa Free Mwakangale Jazz. Alipokuwa huko akakutana na vijana kutoka jimbo la Luanshya waliokuwa  na kundi lao      wakipiga vizuri sana muziki, akaongea nao na hatimae wakakubaliana kuondoka kwao na kuingia Tanganyika kujiunga na Free Mwakangale Jazz, mmoja wa vijana hao alikuwa Michael Enoch. Michael Enoch baadae alikuja kuchukuliwa na Dar es Salaam Jazz Band na kuiendeleza kwa miaka mingi akiwa mpiga solo, kisha akahamia Dar es Salaam International akiwa mpiga saksafon  na hatimae Mlimani Park Orchestra alikoendeleza umahiri wake katika saksafon, na kupewa majina mengi ya sifa, King Enoch, na Teacher, Michael alikutwa na mauti  alipokuwa DDC Mlimani Park Orchestra.
Bendi ya Free Mwakangale Jazz makao yake makuu yalikuwa mji uliopewa jina la Neu Langenburg na Wajerumani lakini wote tunaufahamu siku hizi kama Tukuyu, , pamoja na Michael Enoch bendi hiyo ilikuwa na wanamuziki wengine wanaokumbukwa ni Ben Jack na Saiz Vera.
Kuna hadithi ya kuchekesha na kusikitisha kuhusu kisa kilichofanya Free Mwakangale Jazz ife na Michael Enoch atue Dar es Salaam Jazz Band.
Siku moja  bendi ya Free Mwakangale Jazz ilipata safari ya kwenda Mwanza na baada ya kufika huko ilifanya maonyesho kadhaa, siku moja vijana hawa walikodi gari ili kubeba vyombo vyao, pengine wakati huo kwa ugeni na pengine hata Kiswahili walikuwa hawajakifahamu sawasawa, dreva wa gari akawaomba wamsubiri akaweke mafuta, wakamruhusu, alipoondoka hakuonekana tena ukawa ndio mwisho wa Free Mwakangale Jazz. Wanamuziki wakajikuta wamekwama Mwanza, bahati nzuri baada ya muda mfupi walipata kazi ya kupiga muziki katika bendi moja pale Mwanza, wakiwa katika bendi hiyo, muwakilishi wa Dar es Salaam Jazz Band , marehemu Limi Ally,ambaye alikuwa katika harakati za kumtafuta mpiga gitaa la solo akamuona Michael Enoch, na ndipo wakakubaliana kurudi nae Dar es Salaam kujiunga na Dar es Salaam Jazz Band.

Bendi nyingine ya Mbeya ilikuwa TANU Youth League Jazz Band, bendi iliyokuwa maarufu miaka ya sitini na ilirekodi nyimbo kadhaa RTD, kati ya nyimbo zake zilizokuwa maarufu ni ule ulioitwa Nampenda Firida mwenye macho mazuri. Kulikuwa na bendi nyingine ambayo ilisemekana ilitokana na kufa kwa TANU Youth League Jazz Band ilikuwa ikiitwa  bendi ya Lemi au Remi.

Bendi nyingine iliyokuweko Mbeya ni hiyo iliyoko kwenye picha ambayo iliitwa Azimio Co Bantou Jazz Band. Ukiangalia vizuri picha hiyo, utaona ilipigwa katika kota zilizokuwa za wafanyakazi wa  serikali zilizokaribu na mitaa ya Ghana, pengine hapo ndipo yalikuwa masikani ya bendi hii.

Katika tasnia ya muziki wa bendi kuna utamaduni wa kuigana majina, kwa mfano baada ya kuundwa bendi ya Dar es Salaam International Orchestra, bendi nyingi ziliibuka na kujiita international, zikiwemo Dodoma International Orchestra, Tanga International Orchestra, Ruaha International Orchestra na kadhalika. Kule Sumbawanga ikaundwa bendi iliyoitwa Rukwa International Orchestra, bendi hii ilijitokea sana na kushiriki matukio ya kitaifa. Rukwa International Orchestra ilikuwa mojawapo ya bendi zilizojitokeza kushiriki Mashindano ya Bendi Bora (MASHIBOTA) yaliyofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee Dar es Salaam miaka ya 90.

Saturday, October 2, 2010

Atomic Jazz Band




Atomic ilikuwa moja kati ya bendi zilizowika sana nchi hii. Bendi iliyokuwa na makazi yake Tanga, Tanga wakati huo ikiwa na vikundi vingi maarufu vya muziki, kama vile Jamhuri, White Star, Amboni, Lucky Star, Black Star. Bass katika bendi hii kwa kweli lilikuwa likiingiza upigaji wa bezi katika kiwango kipya,wapigaji wake walileta changamoto hata walipokuja hamia katika bendi mpya. Pichani toka kushoto John Mbula -Saxophone,Rodgers- mwimbaji, John Kilua-Thumba(huyu alikuwa ni ndugu ya Julius Kiluwa ambaye ndiye alikuwa mwenye bendi),John Kijiko-Solo gitaa, Hemed Mganga-rythm gitaa (niliwahi kupiga bedni moja na mzee Mganga kwa wakati fulani. Tulikuwa wote Orchestra Makassy na ndie baba mzazi wa mwimbaji wa kizazi kipya Kassim Mganga),Mohamed Mzee-Bass.
Picha hii ilikuwa ni jarada la santuri iliyokuwa na wimbo maarufu Mado Mpenzi Wangu. Wimbo ulikuwa ni ujumbe wa kweli kutoka kwa mwanamuziki mmoja kwenda kwa mpenzi wake ambae jina kidogo linafanana na Mado ili kuficha ukweli. Mtunzi wa wimbo huu alikuwa mpenzi sana wa bendi hii na bado kwa rafiki zake anajulikana kwa jina la Mado. Siku hizi amekuwa mpenzi tu wa kawaida wa muziki.