Wednesday, December 14, 2022

NI MIAKA 12 TOKA KIFO CHA DR REMMY ONGALA -TUMUOMBEE KWA KUKUMBUKA YALIYOJIRI KATIKA MAZISHI YAKE



Ni miaka 12 toka Dr Remmy alipofariki siku ya Jumapili tarehe 12 Disemba mwaka 2010, kiasi cha saa sita usiku katika hospitali ya  Regency Hospital.  Siku chache kabla ya hapo alikuwa amelazwa Mhimbili akiwa na matatizo ya kisukari na figo, akaonekana amepata nafuu akaruhusiwa kurudi nyumbani, lakini akazidiwa na kupelekwa hospitali ya  Regency, ambako mauti yalimkuta.

Picha za baadhi ya marafiki, na ndugu waliokusanyika nyumbani kwa  Dr Remmy baada ya kusikia msiba  


Cosmas Chidumule  nyuma yake ni Juma Mbizo

Waziri Ally na  Mzee Manyema

Mzee makassy na Mzee Manyema

Mbombo wa Mbomboka

Mohamed Mgoro

Cosmas na Mzee Kungubaya

Mzee Makassy na Waziri Ally

Chiddy Benz na Bombo wa Bomboka

Kally Ongala akiwa na Nyoni, mmiliki wa bendi ya   Super Matimila 

King Kiki akiwa na Shogholo Challi Katibu Mtendaji wa BASATA wakati huo.

Geophrey Kumburu na Farijala Mbutu

Mgosi Mkoloni

 Joseph Mbilinyi aka Sugu

Mohamed Mgoro na Joseph Mbilinyi (Sugu)

Chidumule na Sugu

Hamza Kalala, Mgoro, Chidumule na Sugu

Rashid Pembe, Sugu, Nindi

Tido Mhando , Mgoro

Makassy, Kanku Kelly,  Chidumule



Ratiba ya Mazishi –Alhamisi 16th December 2010

Saa 4 asubuhi –Mwili wa Dr Remmy kutolewa MUhimbili na kuletwa katika viwanja vya Biafra Kinondoni.

 - Maombi

-   Tamasha la muziki (Gospel na rhumba)

-       Kuaga mwili

Saa 8 – Mwili kupelekwa nyumbani kwa marehemu Sinza

Saa 10 – Mazishi katika makaburi ya Sinza

 

Jumatano 15th Disemba 2010  Mkesha wa siku ya mazishi

Seti mbili za vyombo vya muziki vilipangwa nje ya nyumba ya marehemu, na usiku kucha wanamuziki walipiga muziki wakiimba nyimbo nyingi za marehemu na tungo zao nyingine. Kasaloo Kyanga alipanda jukwaani na kuimba nyimbo ambazo walipiga pamoja na marehemu walipokuwa Matimila.


Kadesi mpiga bezi wa zamani wa OSS


Kasaloo Kyanga

Watu wakicheza kumkumbuka marehemu

Mafumu Bilali Bombenga'Super Sax' akipiga Conga




Elly  Chinyama Chiyaza


Mwema Mudjanga, Nkulu Wabangoi, na Kabeya Badu

Makassy Jnr with Mzee Mwema

Mzee Kungubaya



Bushoke Jnr alikuwepo

Mafumu

Malu Stonch

Siku ya mazishi

 Mwili wa Dr Remmy  uliletwa kwenye viwanja vya Biafra kwa gari hili lililosindikizwa na pikipiki mbili za polisi.




Dr Remmy's Coffin



 Mwili ulipofikishwa Biafra, sanduku liliwekwa katika jukwaa maalumu lililokuwa chini ya hema jeupe. Bendi zikaanza kupiga kuomboleza ikiwemo bendi ya Walemavu. Hatimae bendi maalumu ya wanamuziki wa Injili ilipiga wimbo maalumu wa kumlilia Dr Remmy


Watoto na wajukuu wa Dr Remmy







 Kati ya waliohudhuriwa alikuwemo Wazir wa Habari Michezo na Utamaduni Dr Nchimbi, Wabunge wa Kinondoni na Ubungo, Waheshimiwa Iddi Azan na John Mnyika. alikuwepo pia Jaji John Mkwawa, wawakilishi wa BASATA, COSOTA na SHIWATA na wasanii wengi sana,Jambo lililowatoa machozi watu wengi ni pale wimbo alioimba marehemu ulioitwa Siku ya kifo ulipopigwa.







Baada ya hotuba ya Waziri Dr Nchimbi kwa niaba ya serikali na Cosmas Chidumule kwa niaba ya wanamuziki, mamia ya watu walipita mbele ya jeneza kumuaga mpendwa wao.

 Saa nane mwili ukahamia ukumbi wa Kwa Mgiriki, Sinza kwa Remmy ambapo majirani wa marehemu nao walipata nafasi ya kumuaga kabla ya mwili kupelekwa makaburini.

Mazishi







Mke wa Remmy akisindikizwa baada ya mazishi


Kama ilivyopangwa, saa kumi jioni mwili wa DR Remmy ulizikwa Sinza Makaburini. Yakatimia maneno ya wimbo wake wa Siku ya kifo, kuwa <BINADAMU NI NYAMA YA UDONGO>

1 comment:

  1. An incredible historical photographs collection. Congratulations !!

    ReplyDelete