MZEE Kassim Mapili hatunae tena. Habari ilitufikia jioni hii kuwa Mzee aliingia chumbani kwake Jumanne usiku akitokea kuangalia mechi ya Arsenal na Barcelona, na toka alipoingia hakutoka tena, hivyo jioni ya leo majirani walilazimika kutoa taarifa ambapo polisi walivunja mlango wa chumba cha Mzee na kukuta amefariki. Kutokana na hali ya mwili inaonekana alifariki tangu juzi na hali ya mwili si nzuri. Mzee Mapili alilazwa miezi michache iliyopita Muhimbili kutokan na kuwa na tatizo la moyo, lakini alikusema mwenyewe hata wiki iliyopita kuwa kutokana na kusaidiwa na Salma Moshi, msanii mkongwe anaeishi Marekani kupata Bima ya Afya hali yake imeimarika kwani anapata dawa zote zinazohitajika bila ya matatizo. Siku ya Jumatatu Mzee mapili alishiriki kikamilifu katika kumzika mtangazaji Fred Mosha, na hata kumuimbia marehemu akisikitika kuondoka kwake mapema. MUNGU AMLAZE PEMA MZEE WETU MAPILI
Thursday, February 25, 2016
MZEE KASSIM MAPILI HATUNAE TENA
MZEE Kassim Mapili hatunae tena. Habari ilitufikia jioni hii kuwa Mzee aliingia chumbani kwake Jumanne usiku akitokea kuangalia mechi ya Arsenal na Barcelona, na toka alipoingia hakutoka tena, hivyo jioni ya leo majirani walilazimika kutoa taarifa ambapo polisi walivunja mlango wa chumba cha Mzee na kukuta amefariki. Kutokana na hali ya mwili inaonekana alifariki tangu juzi na hali ya mwili si nzuri. Mzee Mapili alilazwa miezi michache iliyopita Muhimbili kutokan na kuwa na tatizo la moyo, lakini alikusema mwenyewe hata wiki iliyopita kuwa kutokana na kusaidiwa na Salma Moshi, msanii mkongwe anaeishi Marekani kupata Bima ya Afya hali yake imeimarika kwani anapata dawa zote zinazohitajika bila ya matatizo. Siku ya Jumatatu Mzee mapili alishiriki kikamilifu katika kumzika mtangazaji Fred Mosha, na hata kumuimbia marehemu akisikitika kuondoka kwake mapema. MUNGU AMLAZE PEMA MZEE WETU MAPILI
Monday, February 22, 2016
LEO NDIO SIKU YA MAZISHI YA RAFIKI YETU NA NDUGU YETU FRED CAMILLIUS MOSHA
RIP FRED MOSHA |
RATIBA YA MAZISHI NI KAMA IFUATAYO;
- SAA 4-5 MWILI UTAPELEKWA NYUMBANI KWAKE CHAMAZI UKITOKEA MUHIMBILI
- SAA 7 MWILI KUPELEKWA KANISA LA RC CHANG'OMBE KWA MISA YA MAZISHI
- BAADA YA HAPO SAFARI ITAANZA YA KUELEKEA MAKABURI YA KINONDONI KWENYE MAKAZI YAKE YA MILELE
- MUNGU MALAZE PEMA PEPONI FRED MOSHA
Tuesday, February 9, 2016
WAKONGWE WA DANSI TANZANIA KATIKA WIMBO WA PAMOJA- MIAKA 50 YA UHURU
VIDEO HII YA WIMBO HUU MIAKA 50 YA UHURU INA KUMBUKUMBU NYINGI. HAPA WAPO PAMOJA JUKWAANI, KASONGO MPINDA NA KABEYA BADU
Thursday, December 3, 2015
Wednesday, December 2, 2015
KASONGO MPINDA CLAYTON HATUNAE TENA
Marehemu Mutombo Audax (kushoto), akiwa na marehemu Kasongo Mpinda
HAKIKA siku hii ni ya simanzi, nimetoka makaburi ya Kinondoni ambapo tumemzika mwanamuziki David Musa Gordon wa Safari Trippers, nafika nyumbani taarifa inakuja kuwa mwanamuziki mwingine mkongwe Kasongo Mpinda Clayton amefariki jioni hii nyumbani kwake Mwananyamala na mwili umepelekwa hospitali ya Mwananyamala.
Mungu Amlaze Pema
Saturday, November 28, 2015
DAVID MUSA AFARIKI DUNIA
Kushoto mwenye miwani David Musa, wa tatu Marijani Rajabu na kulia mwisho Jumanne Uvuruge mtunzi wa wimbo wa Georgina.
Mungu amlaze pema
Monday, November 23, 2015
MFAHAMU MBARAKA YUSUPH MWANAMUZIKI WA NATIONAL PANASONIC NA POWER IRANDA
“NIMEACHANA na muziki wa dansi hivi sasa na nimeamua kugeukia sanaa ya filamu, ambapo sababu kubwa ni kupungua kwa kasi yangu ya ucharazaji gitaa, kutokana na kupata mara mbili kwa nyakati tofauti, ugonjwa wa kupooza.”
Hayo ni maneno ya Mbaraka Yusuph, kati ya wacharazaji mahiri wa zamani wa magitaa yote pamoja na Saxophone, aliyewahi kuzitumikia bendi mbalimbali hapa nchini, zikiwamo, The Smashers, National Panasonic, OSS ‘Power Iranda’, Seven Blind Beats na the Big Africa ya Arusha..ENDELEA HUKU
Hayo ni maneno ya Mbaraka Yusuph, kati ya wacharazaji mahiri wa zamani wa magitaa yote pamoja na Saxophone, aliyewahi kuzitumikia bendi mbalimbali hapa nchini, zikiwamo, The Smashers, National Panasonic, OSS ‘Power Iranda’, Seven Blind Beats na the Big Africa ya Arusha..ENDELEA HUKU
Tuesday, April 28, 2015
Thursday, April 23, 2015
MWANAMUZIKI MKONGWE MUTOMBO LUFUNGULA AUDAX HATUNAE TENA
AUDAX(kushoto) akiwa na Kasongo Mpinda |
Tuesday, April 21, 2015
MWANAMUZIKI WA SIKU NYINGI PAUL GAMA AFARIKI DUNIA
KWA MASIKITIKO MAKUBWA TUMETAARIFIWA KUWA MWANAMUZIKI WA ZAMANI PAUL GAMA AMEFARIKI DUNIA HUKO DODOMA TAREHE 16.4.2015 MUDA WA SAA NNE ASUBUHI. NARUDIA MAKALA HII YA HISTORIA YA PAUL GAMA KADRI ALIVYOTUELEZA MWENYEWE
Paul Daniel Gama |
Paul
Daniel Gama alizaliwa Barabara ya 11 Dodoma (1947). Baba yake alikuwa ni
mwanajeshi wa KAR mwenye asili ya Songea na mama yake alikuwa na asili ya
Usangu alikuwa anafanya kazi
katika
Spokes Mashiyane na filimbi yake |
hospitali ya Mirembe ambayo wakati huo ilikuwa ni hospitali kubwa
ya majeruhi wa vita ya pili ya dunia. Aliingia shule na alipofika darasa la
nne alijikuta akiwa na kipaji kukubwa cha kupiga filimbi, wakati huo wapiga
filimbi walipenda sana kumuiga mpiga filimbi maarufu kutoka Africa ya Kusini
Spokes Mashiyane. Akiwa na wenzie walianzisha kikundi ambacho kilikuwa na
maskani eneo la Mji Mpya pale Dodoma. Vijana hao pia walikuwa wakiiga nyimbo za wanamuziki maarufu wa wakati
huo, kama Salum Abdallah na Cuban
Marimba, pia Salum Zahor na Kiko Kids. Katika kufanya fani yao hiyo kama kitu
cha kujipa burudani waliligusa sikio la
aliyekuwa mwalimu wa Elimu ya Watu Wazima katika Community Center ya
pale Dodoma. Mwalimu huyu aliwasaidia kuwaazimia amplifaya moja kutoka kwenye
bendi nyingine ilikuweko Dodoma wakati huo, The Jolly Sextet Band. Band
iliyokuwa ikimilikiwa na Mkenya mmoja ambaye alifika Dodoma kama mfanya kazi wa
East African Postal and Telecommunication Services, huyu bwana alikuja na vyombo vingi akaanzisha
bendi ambayo mmoja wa wapigaji wake alikuwa Mzee Mnenge ambaye hatimaye alitua
NUTA Jazz Band.
Bongos |
Hiki
kikundi cha Gama na wenzie kilikuwa katika mfumo wa Jazz Band za zamani
ambapo walikuwa na ngoma na filimbi tu,ikisindikizwa na kuimba, lakini waliweza
kukonga nyoyo hata za wanamuziki wengine, na Gama akawa anasakwa na bendi
kubwa iliyokuweko wakati ule Central Jazz band. Alipomaliza darasa la saba tu
ndugu yake aliyeitwa Titus Olaf Gama alimshawishi aingie Central Jazz lakini
hakuwa tena mpiga filimbi bali mpiga Bongos, fani aliyoiweza sana hata kuipenda na hasa baada ya kuwaona
wanamuziki wa NUTA akiwemo Muhidin Gurumo
ambaye wakati huo alikuwa akipiga Bongos na kuimba. Bongos no ngoma
ndogo zilizokuwa muhimu katika kundi wakati huo ambapo hakukuweko na drums wala
tumba. Taratibu akaanza kupata hamu ya kupiga bass, wanamuziki wenzie
walimkatisha sana tamaa kwa kuambiwa kuwa vidole vyake vilifaa sana kwa kupiga
bongos na si kupiga gitaa.
Katika
jitihada zake za kujifunza gitaa la bezi alikuwa kila mara akiwahi mazoezi na
kujaribu kujifunza gitaa la bezi. Hilo lilikuwa gumu mpaka pale bendi ya Lake Jazz Band ilipotembelea Dodoma.
Bendi hiyo wakati huo ikiwa na wanamuziki kama Shem Karenga akiwa anapiga gitaa la bezi, Mzee alum
ambaye alikuwa na ulemavu wa macho, mwanzo alikuwa akipiga gitaa la solo na
baadae akahamia kupiga gitaa la rhythm wakati gitaa solo lilikuja kupigwa na
jamaa aliyeitwa Kally. Kutokana na simulizi ni wazi kuwa wanamuziki wa kutoka
Burundi walikuwa wengi sana nchini wakati huo. Pia katika bendi hiyo alikuweko
Mzee Juma Kitambi, mtunzi wa wimbo maarufu wa Rangi ya Chungwa.
Gama
alichukua nafasi hii kumfuata Mzee Salum ili aweze kumfundisha gitaa. Kwa kuwa
wanamuziki wengine walikuwa wakitoka kwenda kutembea Mzee Salum alibaki
nyumbani na hivyo Gama alichukua nafasi hiyo kumnunulia sigara Mzee Salum ana
kumsihi amfundishe gitaa nae alifanya hivyo na Gama akatokea kuwa mpiga bezi
mahiri.
Katika
kipindi hiki akatokea mfanya biashara Mohamed Omar Badwel, huyu alikuwa na
gereji na studio ya kupiga picha, aliweza kwenda Mombasa na kurudi na seti ya
vyombo na kuanzisha Dodoma Jazz Band. Gama akahama Central Jazz Band na
kujiunga na wanamuziki wengine walioanzisha Dodoma Jazz. Band ilianza ikiwa na
mpiga solo Hassan Mursali mwanamuziki mweny asili ya Malawi, siku hizo ikiitwa
Nyasaland alikuwa ndie mpiga solo, lakini aliwaacha baadae na kujiunga na NUTA
Jazz Band, upigaji wake wa solo unaweza kuusikia katika kusikiliza kibao kimoja
maarufu cha NUTA, kilichoitwa Dunia Njema
Kukaa Wawili.
Hasan
alikuwa mtu wa kuhama hama hatimae alipoteza uwezo wa kusikia jambo ambalo
lilihusishwa na kuhamham kwake kwani ushirikina ulitawala sana wakati huo, kama
maelezo yanayofuata yanavyoonyesha. Dodoma Jazz ilikuwa pia inafanya ziara
katika sehemu nyingi , kama vile Iringa, Mbeya ,Tabora, Dar es Salaam na
kadhalika, lakini safari moja ya kwenda Kilosa ilifanyika ikiwa na lengo la
kumfuata Abel Barthazal aliyekuwa akipiga katika bendi ya Kilosa Jazz.
Bendi ilipokelewa vizuri na wakafanya
maonyesho yao Kilosa na hatimae kuondoka na Abel. Siku chache baade wakati huo
Mzee Mohamed Omar, mwenye bendi
alikuwa kasha mnunulia suti kadhaa Abel, ukaja ugeni toka Kilosa wakiwa na
barua yenye maelezo kuwa ikiwa Abel Hatarudi Kilosa, mmoja wa wanamuziki wa
Dodoma Jazz atafariki, na barua hii ililetwa kwa mkono na mjumbe ambae
alisisitiza wakishaisoma mbele yake ndio anaondoka. Abel alirudishwa Kilosa
mara moja.
Baada
ya hapo aliyekuwa meneja wa bendi Ramadhan Waziri alitumwa Burundi kwenda
kutafuta wapigaji, siku alipokuwa anarudi na wapigaji wapya akakutana kwenye
treni na Rashid Hanzuruni, mpiga solo mahiri sana ambaye upigaji wake husikika
katika wimbo Napenda nipate lau nafasi
Hanzuruni
alikuwa kaiacha Tabora Jazz baada ya
kutokea ugomvi mkubwa ambapo alipoteza meno kadhaa, hivyo alikuwa kwenye
hilo treni akielekea Dar es Salaam kumfuata mpigaji mwenzie Samba ambae alikuwa
NUTA Jazz. Ramadhani aliweza kumshawishi hanzuruni akabaki Dodoma Jazz ambako
alikaa kwa muda na hatimae akaja kuchukuliwa na Sama ili aingie NUTA Jazz,
ndoto hiyo haikufanikiwa kwana NUTA alikuweko mpigaji mahiri Hamisi Franco, hii ndiyo ilipelekea
Hanzuruni kwenda Western Jazz Band
Friday, January 16, 2015
IMETIMIA MIAKA 36 TOKA KIFO CHA MBARAKA MWINSHEHE, MUZIKI WAKE BADO UKO HEWANI
Mbaraka
Mwinshehe Mwaruka alizaliwa mjini Morogoro Juni 27, 1944. Siku ya
Januari 12, 1979 ulimwengu wa muziki Tanzania ulitikiska kwa simanzi
baada ya kusikika kifo cha mwanamuziki huyo, mpiga gitaa muimbaji,
mtunzi na kiongozi wa bendi wa miaka mingi na ambaye bendi yake ilikuwa
imepiga karibu kila wilaya ya nchi hii. Taarifa ziliingia jioni ya siku
ile kupitia redio ya Taifa kuwa nguli huyu alifia katika hospitali
katika jiji la Mombasa nchini Kenya muda wa saa 1:55 jioni kufuatia
ajali ya gari...........ENDELEA HUKU
Tuesday, December 16, 2014
HATIMAE SHEM IBRAHIM KARENGA AZIKWA
HATIMAE
mwanamuziki mkongwe mpiga gitaa muimbaji na mtunzi mahiri Shem Ibrahim
Karenga amezikwa katika makaburi ya Kisutu jioni ya leo. Shughuli hiyo
ilianza kwa utata baada ya kuwa makaburini hapo kulikuwa na misiba minne
hivyo kila lilipokuja jeneza wanamuziki, ndugu na wapenzi wa muziki
walijikuta wakisindikiza jeneza na..........INAENDELEA HUKU
Monday, December 15, 2014
BURIANI SHEM IBRAHIM KARENGA
LEO
Jumatatu tarehe 15 Desemba 2014, majira ya saa nne asubuhi taarifa
zilianza kusambaa kuwa mwamba mwingine wa muziki wa dansi Tanzania
umedondoka. Mzee Shem Karenga hatunae tena,kwa vyovyote waliohudhuria
dansi alilopiga Ijumaa na Jumamosi iliyopita pale Mwembeyanga watakuwa
hawaamini, lakini imekuwa mapenzi ya Mungu, kwamba asubuhi ya leo
aliamka hajisikii vizuri na alipelekwa hospitali ya Amana lakini
hakukuweza kufanyika kitu Mzee akarudi kwa Muumba wake. Mungu aipokee
roho yake. Miezi michache iliyopita tulipata muda mrefu wa kuongea na
Mzee Shem Karenga ili kujua alikotokea na mawazo yake kwa sasa
mazungumzo yalikuwa kama ifuatavyo;................................. ENDELEA HUKU
Subscribe to:
Posts (Atom)