Tuesday, April 12, 2022

MWAKA 1973 YALIFANYIKA MASHINDANO YA BENDI BORA TANZANIA UNAJUA MSDHINDI ALIKUWA NANI?

 

TANGAZO la mashindano hayo lilitolewa kwenye gazeti na mashindano hayo yalidhaminiwa na NDC.. Shirika la Maendeleo la Taifa.

Mshindi wa kwanza ilikuwa ni bendi ya Sunburst. Picha ya chini kulia, aneonekana amevaa kofia na kushika kikombe ni James Mpungo kiongozi wa Sunburst, bendi ya pili ilikuwa Tonics na Marijani Rajabu akiwakilisha Safari Trippers iliyochukua zawadi ya tatu







Hawa ndio Sunburst bendi iliyoanzishwa mwaka 1970 na mwanamuziki Mkongo Hembi Flory, ilikuwa bendi moto sana mwanzoni mwa miaka ya 70. Mwaka 1973 ikashinda mashindano ya Bendi Bora Dar es Salaam na kuwa ya kwanza. Katika picha hapo juu, toka kushoto Toby John Ejuama (saxophone) huyu alikuwa Mnaijeria kutoka Biafra, kama mnakumbuka Tanzania tulimuunga mkono  Ojukwu, kiongozi aliyekuwa na ndoto za jimbo la Biafra kujitenga na Nigeria, hivyo tukawa kimbilio la watu kutoka huko. Anaefuata ni Flory mpiga gitaa Mkongo, kisha mkongwe Johnny Rocks kwenye (drums), huyu alikuwa pia anapiga na George Di Souza pale Margot.  James Mpungo (lead vocals) kijana wa Mbeya ambaye hatimae alijiunga na Mangelepa. Anafuatia Kassim Rajabu Magati (organ/lead vocals, kwenye gitaa la bezi ni Bashir Idd Fahani. 



No comments:

Post a Comment