Tuesday, April 2, 2013

HATA MBUYU ULIANZA KAMA MCHICHA

FRANCO LUAMBO LUANZO MAKIADI (RIP)

2 comments:

  1. Mwenyewe....Franco!!! Juzi hapa nilikua natazama sinema moja ndiyo imetoka karibuni kuhusu mashindano ya ngumi baina ya Muhammad Ali na George Foreman, mjini Kinshasa 1974. Enzi hizo hatukua na TV Bongo tuliambulia tu kusikia redioni. Lakini mbali na sinema mbili zilizotoka (When we were Kings na Ali- nadhani 2002) kuna filam ya wanamuziki waliotumbuiza shughuli hiyo. Akina James Brown, BB King, Sister Sledge ( waimbaji wa We Are The Family), nk. Sasa Afrika waliowakilisha ni Miriam Makeba (ukimwona huyu mama enzi hizo mbiiiichi, bado kijana- utahisi damu inakupanda), Tabu Lei na Mzee Luambo Makiadi---yaani huyu Franco. Yeye na Tabu Lei ndiyo walikua kama Simba na Yanga wa muziki Zaire miaka hiyo. Kibonge cha sinema. Inaitwa "Soul Power" (2008) kwa wenye uwezo inauzwa Amazon, bei chee kabisa...

    ReplyDelete
  2. Namuheshimu sana marehemu Franco, lakini nadhani kama kuna mpiga gitaa aliyetoa mchango mkubwa sana katika muziki wa Congo katika miaka ya 70 na 80 ni mpiga solo Felix Manuaku Waku, maarufu kama Pepe Fely, mmoja wa waanzilishi wa Zaiko Langa Langa. Huyu anajulikana kama 'father of the modern Congolese guitar', yaani baba wa gitaa la kisasa la Congo. Wapiga gitaa kama Diblo Dibala, Dally Kimoko, Alain Makaba na Nene Tchakou wanajaribu kufikia japo nusu tu ya kile alichokuwa akikifanya wa Pepe Fely. Huyu jamaa ni mchawi. Hebu Kitime embed video hizi za YouTube humu na watu wataelewa nina maana gani. /watch?v=KLpThsPQ6G0 (hii yupo na Grand Zaiko mwanzoni mwa miaka ya 80); /watch?v=idZDt2RUtIk na /watch?v=uYgtOTWnZ1Y (hizo yupo na Zaiko Langa Langa miaka ya 70). Hizi zote ni live.

    ReplyDelete