Thursday, May 8, 2014

DDC MAGOMENI WAVUNJWA RASMI

Kumbi za DDC zilikuwa maarufu sana katika jiji la Dar katika miaka ya 80. Kulikuweko na kumbi za DDC Kariakoo, DDC Magomeni, DDC Keko, zikuwa maarufu kwani wakati huo kulikuwa na uhaba mkubwa wa bia, lakini katika kumbi hizi bia zilikuwa hazikauki, Pia zilikuwa kumbi maarufu kwa madansi na matukio makubwa yakiwemo masumbwi. DDC Magomeni ulikuwa kituo kikubwa cha burudani. Wiki hii ukumbi huo umepigwa nyundo na pamebaki uwanja mtupu ambao kunaelekea kutajengwa kitu. Kuna uwezekano mdogo sana kuwa nafasi hiyo itajengwa tena kwa ajili ya burudani bye bye DDC Magomeni, mengi makubwa ya muziki yalifanyika pale.

No comments:

Post a Comment