Tuesday, June 27, 2017

BROTHER ZENNO AFARIKI DUNIA

RIP Brother Zerno
Hakika siku za karibuni zimekuwa ngumu kwa wapenzi wa muziki wa zamani, mfululizo wa misiba na wanamuziki kuugua kumekuwa ni habari karibu kila siku. Mchambuzi mahiri wa muziki wa Charanga Zerno Andrew Lucas, aliyefahamika zaidi kwa jina Brother Zeno, amefariki dunia asubuhi leo katika hospitali ya Temeke,  Brother Zeno  aliyekuwa akishirikiana na 'Mzee wa Macharanga' Charles Hillary enzi hizo Radio One, alikuwa na ufahamu mkubwa wa muziki wa kutoka Cuba na hivyo kuwa mpenzi mkubwa wa watu waliopenda muziki huo. Brother Zeno amesumbuliwa karibu mwaka mzima na tatizo la moyo na katika siku zake za chache mwisho alikuwa akipumua kwa msaada wa mashine, alitegemewa angepata nafuu na kuhamishiwa Muhimbili kwa matibabu zaidi lakini Mungu amekuwa na mipango mingine.
Msiba wa Mzee utakuwa nyumbani kwake Mbagala Kibonde Maji na mazishi yatakuwa kesho 28/6/2017 saa kumi hukohuko Mbagala

No comments:

Post a Comment