Mwanamuziki mkongwe katika Taarab Fatuma Bint Mbaraka
maarufu kwa jina la Bi Kidude
amefariki dunia muda mchache uliopita huko Bububu Zanzibar, sehemu alikokuwa
anaugulia kwa kipindi sasa. Mwili wake utahamishiwa kwake Rahaleo na mazishi
yatakuwa kesho. Bi Kidude alizaliwa katika kijiji cha Mfagimaringo, alikuwa
binti wa mchuuzi wa nazi, hakuna anayejua haswa Bibi huyu alizaliwa tarehe
ngapi, kuna hata mawazo kuwa alikwishafikisha miaka 102.

Bi Kidude pia liwahi kuimba na Sitti Binti Sadi wakati wa
ujana wake, na katika maisha yake Bi Kidude amekwisha zunguka mabara yote
akiimba katika majukwaa na wanamuziki maarufu ulimwenguni
Mungu Amlaze Pema Peponi Bibi yetu. Amen
No comments:
Post a Comment