Thursday, June 29, 2017

HATIMAE MWANAMUZIKI MKONGWE BROTHER ZENNO AZIKWA

MWANAMUZIKI  na mchambuzi wa muziki wa charanga maarufu kwa jina la Brother Zeno hatimae amezikwa na makaburi jirani na alipokuwa akiishi kule Mbagala Kibondemaji. Zerno ambaye alikuwa muimbaji mzuri atakumbukwa kwa kuwa mmoja wa waanzilishi wa bendi ya Dar es Salaam Jazz B, bendi iliyokuwa ikiongozwa na Patrick Balisidya, ambayo ilianza kufanikiwa kwa kasina kuanza kuwa tishio kwa Dar es Salaam Jazz Band A, chini ya Michael Enoch, bendi ikavunjwa na wanamuziki wengine wakaingizwa Dar Jazz A, lakini Patrick akakasirika na kutokomea , baadae akaja kuanzisha Afro 70 na kufanya mambo makubwa. Baadae Brother Zeno alijiunga na Shirika la Bima ya Taifa, na baada ya kujiunga kampuni hiyo ndie aliyetoa msukumo wa kuanzishwa kwa bendi katika shirika hilo, Bima Jazz Band na hivyo pia kupewa kazi ya kutafuta wanamuziki wa kujiunga na bendi hiyo na yeye mwenyewe kuwa kati ya wanamuziki waanzilishi wa kundi hilo lililokuja kujizolea umaarufu mkubwa. Kati ya wanamuziki wa kwanza katika bendi hiyo waliobaki hai sasa ni wawili tu baada ya kifo cha Zeno. 







Binti pekee wa marehemu akiwa na mumewe wakiweka shada la maua







Baadhi ya wanamuziki waliohudhuria mazishi ya Brother Zeno


Aliyekaa ni Abdallah Mbosanga mmoja ya wanamuziki wawili waliobaki hai wa bendi ya Bima Jazz band ya kwanza. Mwingine ni Duncan Ndumbalo

No comments:

Post a Comment